Search This Blog
Thursday, July 2, 2020
Zoezi la kutafuta miili ya watu kwenye mgodi wa madini nchini Mynamar lasitishwa
Zoezi la kutafuta miili ya watu waliokwama kwenye mgodi wa madini ya Jade nchini Mynamar limesitishwa kufuatia mvua kumbwa zinazoendelea kunyesha na hivyo kuzuia kupatikana kwa watu waliokwama na ambao huenda tayari wamepoteza maisha kutokana na tope linalozidi kuporomoka na kufanya zoezi hilo kuwa gumu.
Mpaka sasa miili ya watu 113 pekeendio imekwishapatikana ambapo Polisi wa eneo hilo wamesema, wachimbaji hao walikaidi onyo la kutofanya kazi katika migodi hiyo wakati wa mvua.
Msemaji wa kikosi cha uokoaji nchini Myanmar Than Win Aung, amesema vifo vingi zaidi vingeripotiwa endapo wasingechukua hatua ya kuwaonya wachimbaji waliokuwa katika mgodi uliopo kaskazini mwa nchi hiyo.
Taarifa zinasema, Mgodi huo uliporomoka na kuwafunika wachimbaji hao kwa tope zito baada ya mvua kubwa kunyesha karibu na mpaka wa China katika jimbo la Kachin.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment