Search This Blog
Friday, July 31, 2020
Waziri Mkuu: Wanasiasa Waeleze Watakayo Fanya Kuliko Kubeza Yaliyofanyika
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amewataka wanasiasa kufanya kampeni za kistaarabu mara kampeni za Uchaguzi Mkuu zitakapofunguliwa ili kuepuka vurugu zinazoweza kusababisha uvunjifu wa amani
Majaliwa amesema ni muhimu kwa wanasiasa kueleza yale waliyopanga kuwasaidia wananchi kuliko kubeza yale yaliyofanywa na wengine na kukashfu
Amefafanua, “Tujiepushe na lugha za uchochezi, tujiepushe na lugha za kubeza, tujiepushe na lugha za kashfa, kazungumze kile ambacho utawatendea wananchi”
Amewashukuru viongozi wa dini kwa kuendelea kuimarisha amani na mshikamano nchini kwa kutoa mawaidha yenye kujenga
Aidha, amemuagiza Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Aboubakar Kunenge kuunda Tume maalum kuchunguza matukio ya kuungua kwa moto mfululizo kwa shule za msingi na Sekondari zinazomilikiwa na taasisi za dini ya Kiislamu nchini
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment