Search This Blog
Wednesday, July 8, 2020
Wananchi wa jimbo la Nanyamba wameshauriwa kuimarisha ulinzi na usalama katika maeneo yao
Na Faruku Ngonyani, Mtwara.
Wananchi wa jimbo la Nanyamba Halmashauri Mkaoni Mtwara wameshauriwa kuimarisha ulinzi shirikishi na usalama katika maeneo yao ili kuepukana na matendo ya uvunjifu wa amani.
Wito huo umetolewa na mbunge wa Jimbo hilo Abdallah Dadi Chikota alipokuwa anazungumza na wananchi hao katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji cha Mnongodi ndani ya Halmashauri hiyo.
Chikota alisema kuwa na ni vyema kwa wananchi hao wakawa makini na wageni wanaoingia katika maeneo hayo kwani kijiji hiko kimekaribiana na vijiji vilivyopo nchi ya jiyani.
“Niwaombe wananchi wangu kwa sasa inatakiwa muimarishe ulinzi shirikishi wenyewe kwani suala hili la ulinzi linaanza na sisi wenyewe wanachi”Alisema chikota.
Chikota amekuwa mbunge wa kwanza toka kuanzishwa kwa Jimbo la Halmashauri ya Mji wa Nanyamba lilianzishwa mwaka 2015 kutoka kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano anayeshughulikia Sekta ya Ujenzi, Arch. Elius Mwakalinga, akitoa maelekezo kwa Kai...
No comments:
Post a Comment