Search This Blog
Wednesday, July 22, 2020
Timu ya Fenerbahce ya Uturuki Yamtaka Mbwana Samatta
Kwa mujibu wa gazeti la habari za michezo la Nchini Uturuki la Takvim limeripoti kuwa klabu ya Fenerbahce ya Uturuki inavutiwa na mshambuliaji mpya wa Aston Villa ya England, Mbwana Samatta.
Mshambuliaji huyo raia wa Tanzania alijiunga na Villa katika dirisha la usajili lililopita akiwa chaguo la kwanza ili kuziba pengo la Mbrazil, Wesley aliyekuwa akisumbuliwa na majeraha.
GENK, BELGIUM – AUGUST 22 : Ally Mbwana Samatta forward of KRC Genk, Philippe Clement head coach of KRC Genk during a press conference before the UEFA Europa League Play-Offs 1st Leg match between KRC Genk and Brondby IF on August 22, 2018 in Genk, Belgium, 22/08/2018 ( Photo by Vincent Kalut / Photonews
via Getty Images)
Samatta ameshindwa kuleta mafanikio ndani ya Aston Villa katika michezo yake ya Premier League baada ya kufunga goli moja 1 pekee katika michezo 12 aliyocheza.
Kwa mujibu wa Takvim, Fenerbahce inakaribia kumnasa Samatta kutokana na hali iliyopo kwa sasa ndani ya Aston Villa na itawakilisha ofa yake ya kumchukua kwa mkopo kutoka katika klabu hiyo ya Birmingham.
Inadaiwa yapo makubaliano ya maneno baina ya Samatta na Villa kuwa Aston Villa itatakiwa kumruhusu kujiunga na klabu nyingine endapo timu hiyo haitafanikiwa kuwepo Premier League katika msimu ujao.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment