Rapa machachari asiyeishiwa vituko kutoka pande za Brooklyn Marekani, Tekashi 69 anatarajia kuwa mtu huru kabisa, ambapo Leo Julai 30, anakua kabakiza siku tatu pekee kumalizia kifungo chake cha nje ambacho amekua akitumikia nyumbani kwake kwa muda wa miezi minne iliyopita.
Itakumbukwa, kwa karibu miaka miwili sasa rapa huyo amekua kifungoni kutokana na hukumu aliyoipata baada ya kupatikana na hatia ya makosa tisa ikiwemo kufanya malipo na umiliki wa silaha za moto makosa ambayo yangemfanya #Tekashi atumikie miaka 32 nyuma ya nondo, lakini Disemba 18, 2019, #Tekashi alipunguziwa hukumu na kufikia miezi 24 baada ya kutoa ushirikiano kwa serikali.
Muwakilishi kutoka upande wa 6ix9ine amethibitisha kuwa rapa huyo anatarajiwa kuachiliwa rasmi Jumapili hii Agosti 2.
Sanjali na hilo, mtandao wa Page Six umeripoti kuwa, kwasasa #Tekashi ataimarisha ulinzi wake zaidi pindi atakapokuwa huru uraiani.
Search This Blog
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment