Wamiliki wa Viwanda Wilaya za Dodoma na Bahi watakiwa kuwa na utamaduni wa kufanya ukarabati wa mara kwa mara na kubadili vifaa vilivyo tumika kwa muda mrefu ili kuepuka gharama zisizo za lazima na matumizi makubwa ya nishati ya umeme.
Wito huo umetolewa hivi karibuni na Mhandisi Mtafiti wa TANESCO, Aurea Bigirwamungu wakati wa kutoa elimu juu ya matumizi bora ya Nishati ya Umeme katika wilaya za Dodoma na Bahi.
Aidha Bigirwamungu ameshauri wamiliki hao kuwa na utamaduni wa kubadilisha moto za kuendeshea mitambo yao katika uzalishaji ili kutumia nishati ya umeme inayoendana na gharama ya matumizi sahihi ya nishati ya umeme katika viwanda vyao.
Naye Afisa Tawala wa Kampuni ya Nyanza Road Workers, Bakari Mugini amesema kuwa mafunzo hayo wamefahidika kwa kujua matumizi vyema ya umeme ili kuendana na matumizi sahihi ya nishati ya umeme katika kampuni hiyo.
Mugini ameeleza kuwa katika mafunzo hayo wamepata elimu juu ya usalama wa miundombinu iliyopo katika viwanda ili kuongeza uzalishaji katika shughuli za kampuni zao.
“Kipekee nalipongeza shirika la TANESCO kwa utendaji bora juu ya kusambaza nishati ya umeme na kutoa huduma bora kwa wananchi na kuhakikisha umeme Mkoani Dodoma unakuwa wakutosha na unapatikana bila matatizo na kama kna tatizo basi wananchi mnataarfiwa awali na baada ya marekebisho ya kiufundi umeme unarejea na shughuli zinaendelea “, ametoa pongezi Mugini.
Search This Blog
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment