Search This Blog
Thursday, July 9, 2020
Rais Magufuli afanya uteuzi wa DC, Mkurugenzi na makatibu Tawala wa wilaya mbili
Rais Magufuli amemteua Kamanda wa Kikosi cha Polisi TAZARA, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Advera John Bulimba kuwa Mkuu wa Wilaya ya Nzega akichukua nafasi ya Godfrey William Ngupula
Aliyekuwa Afisa Mipango wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe, Solomon Isack Shati ameteuliwa kuwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Hanang akichukua nafasi ya Bryceson Paul Kibasa
Aidha, Waziri wa Utumishi, Kept (Mst) George Mkuchika kwa mamlaka aliyokasimiwa na Rais Magufuli amemteua Omary Mwanga kuwa Katibu Tawala Wilaya ya Nachingwea akichukua nafasi ya Husna Juma Sekiboko
Pia, Waziri Mkuchika amemteua aliyekuwa Afisa Tarafa Wilayani Mbulu, Saitoti Zelothe Stephen kuwa Katibu Tawala Wilaya ya Mbeya akichukua nafasi ya Hassan M. Mkwawa
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment