Search This Blog
Saturday, July 11, 2020
Master J Kumuoa Shaa Mwaka Huu "Pole Sana Mpenzi Wangu Kwa Kuvumilia Miaka 15 Mpaka Isidingo Imeisha"
Wataalamu wa mambo wanasema Master J na Shaa ni miongoni mwa Wachumba waliokaa kwenye uchumba kwa miaka mingi zaidi, pamoja na hayo kuna good news mwaka huu na ameisema Master J mwenyewe.
Producer huyo Mkongwe wa Bongofleva ameyasema haya “Naomba niseme ukweli, mwaka huu naoa kwa sababu tayari Mahakamani nimeshamaliza maswala ya mkataba kuvunja ile ndoa yangu ya kwanza kwahiyo Mwaka huu Mungu akijalia nafanya kweli”
“Hatimaye……….. na namshukuru sana Shaa kwa kunivumilia muda wote huu karibu miaka 15….. hata Isidingo si imeshaisha… hahahhhhhahahaaha, samahani sana na pole sana Mpenzi wangu” amesema Master J
Mara ya kwanza wawili hawa kukutana ilikua ni wakati Shaa alipokwenda Studio kwa MJ kurekodi wimbo wao wa kundi uitwao ‘hoi’ hiyo ndio ilikua mara ya kwanza kukutana nae kisha wakaenda South Africa kumalizia kurekodi,
“Tukaanza kuzoeana na kuwa karibu sababu tulikua tuko pamoja muda mwingi tukifanya kazi kila siku” amemalizia Master J.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment