Search This Blog

Saturday, July 11, 2020

Master J Kumuoa Shaa Mwaka Huu "Pole Sana Mpenzi Wangu Kwa Kuvumilia Miaka 15 Mpaka Isidingo Imeisha"


Wataalamu wa mambo wanasema Master J na Shaa ni miongoni mwa Wachumba waliokaa kwenye uchumba kwa miaka mingi zaidi, pamoja na hayo kuna good news mwaka huu na ameisema Master J mwenyewe.

Producer huyo Mkongwe wa Bongofleva ameyasema haya “Naomba niseme ukweli,  mwaka huu naoa kwa sababu tayari Mahakamani nimeshamaliza maswala ya mkataba kuvunja ile ndoa yangu ya kwanza kwahiyo Mwaka huu Mungu akijalia nafanya kweli”

“Hatimaye………..  na namshukuru sana Shaa kwa kunivumilia muda wote huu karibu miaka 15….. hata Isidingo si imeshaisha… hahahhhhhahahaaha,  samahani sana na pole sana Mpenzi wangu” amesema Master J

Mara ya kwanza wawili hawa kukutana ilikua ni wakati Shaa alipokwenda Studio kwa MJ kurekodi wimbo wao wa kundi uitwao ‘hoi’ hiyo ndio ilikua mara ya kwanza kukutana nae kisha wakaenda South Africa kumalizia kurekodi,

“Tukaanza kuzoeana na kuwa karibu sababu tulikua tuko pamoja muda mwingi tukifanya kazi kila siku” amemalizia Master J.

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...