Search This Blog
Thursday, July 30, 2020
Kizimbani Kwa Kuwaingizia VIDOLE Sehemu za Siri Watoto Wadogo 7
Irene James (36) amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Tabora akituhumiwa kuwafanyia unyanyasaji wa kingono watoto 7 wa kike wenye umri kati ya miaka 4 hadi 7 kwa kuwaingizia vidole sehemu za siri
Mtuhumiwa huyo aliwatendea makosa hayo watoto wa majirani zake kwa nyakati tofauti majira ya mchana kati ya Januari hadi Julai mwaka huu katika Kata ya Kanyenye
Makosa hayo ni kinyume cha Kifungu cha 138 C (1) (a) na Kifungu kidogo cha 2(b) cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu Sura ya 16 kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2019
Kutokana na Sheria hiyo Mtuhumiwa akipatikana na hatia atawajibika kwa kifungo kisichopungua miaka 25 na kisichozidi miaka 30 na pia atalipa fidia kwa kiwango kitakachoamriwa na Mahakama
Aidha, Mahakama hiyo imemnyima dhamana mshtakiwa kwa madai ya usalama wake na kwamba amepelekwa mahabusu mpaka pale kesi hiyo itakapotajwa tena Agosti 13
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment