Search This Blog
Sunday, July 5, 2020
Jokate Amtaka Mkurugenzi Apungzue Gharama
Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Jokate Mwegelo amemtaka Mkurugenzi kuweka mazingira mazuri ikiwemo kupunguza bei ya maeneo ili kutoa fursa kwa wawekezaji wanaotaka kuwekeza ndani ya wilaya hiyo waweze kumudu gharama.
Jokate ameyasema hayo katika kikao cha Baraza la Wafanyabiashara wilayani humo, baada ya Afisa Biashara wa Halmashauri ya Kisarawe Joachim Costa kuwasilisha ripoti ya biashara ikionyesha zaidi ya biashara 180 zenye thamani ya shilingi milioni 9 na laki 3 zimefungwa wilayani Kisarawe katika kipindi cha kuanzia mwaka 2019 hadi 2020.
''Tutajitoa kushirkiana na wafanyabishara na wawekezaji wetu, mtu akija hapa hahitaji kukuta vizingiti vingi vya yeye kufanya uwekezaji, hivyo Mkurugenzi angalia maeneo mengine ambayo mtu atatumia gharama za chini kabisa kwasababu lengo letu ni kuvutia wawekezaji'', amesema Jokate.
Aidha Afisa Biashara alibainisha kuwa sababu za biashara hizo kufungwa ni wateja kushindwa kumudu gharama kwenye bidhaa zinazozalishwa Kisarawe pamoja na kuvunjwa kwa miundombinu kwaajili ya kupisha upanuzi wa barabara hali inayopelekea kuathiri biashara nyingi wilayani humo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment