Search This Blog
Tuesday, July 28, 2020
Idris Sultan Asomewa Upya Mashtaka
MSANII wa Vichekesho, Idriss Sultan (27) na wenzake wawili wamesomewa upya mashitaka ya kuchapisha maudhui bila leseni ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) baada ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kumuachia na kumkamata tena.
Mbali na Sultan ambaye ni Mkazi wa Mbezi Beach washitakiwa wengine ni Dokta Ulimwengu (28) Mkazi wa Msasani na Isihaka Mwinyimvua (22) Msanii na Mkazi wa Gongo la Mboto.
Washitakiwa hao awali walifikishwa mahakamani hapo na kusomewa mashitaka hayo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi ambae awali alifuta kesi hiyo na washtakiwa walikamatwa na kusomewa upya mashtaka hayo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment