Search This Blog

Sunday, July 12, 2020

Diamond “Hakuna Uchaguzi Mwepesi Kama Wa Mwaka Huu”


Mwanamuzki Naseeb Abdul (Diamond) amesema kuwa hakuna uchaguzi mwepesi kwenye historia ya nchi hii kama uchaguzi unaotarajiwa kufanyika mnamo mwezi oktoba mwaka huu.

Akizungumza wakati  akitumbuiza kwenye hafla ndogo iliyoandaliwa na rais John Magufuli kwa wajumbe wa mkutano mkuu kutembelea kwenye eneo la ikulu ya Chamwino jijini  Dodoma.

“Mimi nilingundua mapema ndo maana nilianza kumuimba rais Magufuli kabla hata ya uchaguzi maan anajivunia na najua hakuna uchanguzi mwepesi kama huu wa mwaka huu yaani mapema tu tunashinda ” amesema Diamond.

Mapema jana wajumbe wa mkutano mkuu wa chama hicho kilimchangua Dkt John Magufuli na Dkt .Hussen Mwinyi kuwakilisha chama hicho kwenye uchaguzi mkuuu wa mwezi oktoba.

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...