Search This Blog
Monday, July 6, 2020
CCM Yaipongeza Serikali Kwa Kusimamia Uchumi Imara Na Jumuishi Uliopelekea Tanzania Kuingia Uchumi Wa Kati Duniani
Chama Cha Mapinduzi kimeipongeza Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Chini ya Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwa usimamizi wa Uchumi imara, madhubuti na jumuishi ambao umewezesha kuingia katika kundi la nchi zenye uchumi wa kati miaka mitano kabla ya wakati.
Katibu wa NEC – Itikadi na Uenezi ameyasema hayo jana tarehe 04 Julai 2020 Katika Mkutano Mkuu Maalum wa Vyuo na Vyuo Vikuu Mkoa wa Dodoma na uliyohudhuriwa na maelfu ya vijana jijini Dodoma.
Ndg. Polepole anaeleza ni kwa namna gani Sera za CCM zimeelekeza shughuli za maendeleo zilenge kuwatoa wananchi kutoka Tabaka la umaskini na kuishi katika maisha ya staha, utu na kuwezesha ushiriki wao kwenye uzalishaji, biashara na masoko pamoja na fursa jumuishi kwa vijana na wanawake wa kipato cha chini.
Maamuzi makubwa yamefanyika yaliyopelekea uchumi imara yaliyokwenda sambamba na maamuzi ya kimkakati na sahihi kwenye sekta ya madini, usafiri na usafirishaji, viwanda na biashara na sekta nyingine nyingi.
Aidha Polepole amemshukuru na kumpongeza Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwa miaka mitano ya kazi kubwa ambayo mafanikio yake yanaonekana na kupelekea kuvuka kwa haraka kulekea uchumi wa kati tofauti na ilivyotarajiwa kwenye Dira ya Maendeleo ya Taifa iliyolenga kufika huko mwaka 2025.
Chama Cha Mapinduzi kimeridhishwa na Utekelezaji wa ilani ya Uchaguzi Mkuu kwa Mwaka 2015 – 2020 na kuingia katika uchumi wa kati ikiwa ni moja ya utekelezaji wa maono ya Chama Cha Mapinduzi na Serikali yake.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment