Search This Blog

Wednesday, July 15, 2020

Bulaya, Matiko na Mdee washinda kura za maoni za Ubunge


Mshindi wa uchaguzi kwenye kura za maoni za Ubunge CHADEMA Jimbo la Bunda Mjini ni Ester Bulaya mwenye kura 126, Bulaya alikuwa Mgombea pekee na alihitaji tu kura za Ndio au Hapana, kwenye kura 128 zilizopigwa Ndio ni 126 na Hapana 2, hakuna kura iliyoharibika.

Mshindi wa uchaguzi kwenye kura za maoni za Ubunge CHADEMA Tarime Mjini ni Esther Matiko mwenye kura 80 (97. 6%), Matiko alikuwa Mgombea pekee na alihitaji tu kura za Ndio au Hapana ambapo amepata Ndio 80 (97.6) na Hapana 2 (2.4%).

Mshindi wa uchaguzi kwenye kura za maoni za Ubunge CHADEMA Jimbo la Kawe ni Halima Mdee mwenye kura 63 (71.5%) akifuatiwa na Doricus Mwilafi mwenye kura 13 (14.7%), Joel Mwakalebela kura 7 (7.9%) na Felsta Njau  kura 5 (5.6%)

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...