Search This Blog
Thursday, July 23, 2020
Bodi Ya Mikopo Yatoa Ufafanuzi Wanafunzi Kupunguziwa Fedha
Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu Tanzania (HESLB), kupitia Mkuu wake wa Kitengo cha Mawasiliano Omega Ngole, imetoa ufafanuzi kuhusu kupungua kwa kiwango cha fedha za kujikimu kwa wanufaika.
Akizungumza na EATV Omega Ngole amesema kuwa pesa hizo hazijapungua isipokuwa zimetolewa kihalali kama ilivyo muongozo wa Bodi unavyoongoza ambao unataka mwanafunzi kulipwa fedha hizo kipindi anapokuwa shuleni pekee na si vinginevyo.
“Malengo ya fedha hizi ni kunufaisha wanafunzi ili kuongeza wasomi wengi nchini, pesa zinalipwa kulingana na muongozo na ratiba ya chuo husika, kama chuo kikisema utakaa chuo kwa siku ishirini utapatiwa pesa ya siku ishirini bila upungufu wowote, lakini kinachotokea hapa ni mwanafunzi anataka alipwe hadi muda ambao yuko likizo", amesema Omega.
Ameongeza kuwa, “Mara nyingi mwaka wa kwanza huwa wanakuwa na wiki nzima ya kuwahi chuo kufanya maandalizi ya awali , hivyo wataona fedha inakuwa imezidi kwa sababu tunaongezea ile wiki, na anaporudi mwaka wa pili lazima aone mabadiliko, hakuna anayedhulumiwa utalipwa kulingana na ratiba ya chuo watu wasipotoshane”.
Omega amesema kuwa zaidi ya wanafunzi laki moja na elfu arobaini na tano, wanatarajia kunufaika na Mikopo ya Elimu ya Juu kwa mwaka 2020/2021, ambapo elfu hamsini na nne ni wanafunzi wa mwaka wa kwanza.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment