Search This Blog
Sunday, June 28, 2020
Watu za zaidi ya 500,000 wamekufa kutokanakwa Covid-19 duniani huku Texas hali ikiwa ni ya kutisha
Zaidi ya watu 500,000 duniani kote wamepoteza maisha yao kutokana na mlipuko wa virusi vya corona, kwa mujibu wa chuo kikuu cha Johns Hopkins University nchini Marekani.
Tangu mlipuko wa virusi hivyo nchini China mwishoni mwa mwaka jana, kumekuwa na wagonjwa zaidi ya milioni 10, kulingana na Johns Hopkins.
Nusu ya maambukizi yote yalikua yametokea nchini Marekani na Ulaya lakini sasa ugonjwa wa corona inaendelea kukua kwa kasi nchini Marekani.
Virusi hivyo vimeathiri Asia ya kusini na Afrika ambako kunatarajiwa kuwa na maambukizi mpaka mwishoni mwa Julai.
Mlipuko huo bado unaenea katika maeneo mengi ya dunia, kesi mpya zilizorekodiwa kwa siku sita zikiwa milioni moja.
Waandamanaji walishikiliwa katika mji wa Austin, Texas, kwa kukiuka maagizo ya kuvaa barakoa
Marekani imeripotiwa kuwa na jumla ya maambukizi milioni 2.5 na vifo 125,000 vilivyotokana na Covid-19 mpaka sasa na maambukizi zaidi katika nchi nyingine.
Majimbo ya Marekani ambayo yalikuwa yamefunguliwa wiki za karibuni haswa upande wa kusini , yameripotiwa kuwa maaambukizi yameongezeka.
Ongezeko la maambukizi mapya limeonekana zaidi huko Texas, Florida na majimbo mengine ambapo imewabidi kuweka tena zuio la biashara kuendelea.
Takwimu zinaonyesha mataifa kadhaa kutoka bara la Asia na waafrika wanaweza kupata maambukizi zaidi ya mataifa ya wazungu.
Nchi ambayo ni ya pili kuwa na wagonjwa wengi Brazil, taifa hilo lina wagonjwa milioni 1.3 na vifo vinavyozidi 57,000.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment