Search This Blog

Saturday, June 6, 2020

Wagonjwa wa Corona Kenya Wafika 2474 baada ya Wengine 134 Kuongezeka

Katibu wa Wizara ya Afya Mercy Mwangangi ametangaza Ijumaa kuwa idadi ya waliothibitishwa kuambukizwa ugonjwa wa Covid-19 nchini Kenya imeongezeka na kufikia 2,474.

Akitoa taarifa ya kila ya siku kutoka kwa wizara kuhusu maambukizi mapya, Dkt. Mwangangi amesema watu 3,177 wamepimwa katika kipindi cha saa 24 zilizopita huku 134 wakithibitishwa kuambukizwa virusi vya corona.

Wizara hiyo imeongeza kwamba watu 90, 875 wamefanyiwa vipimo nchini Kenya hadi kufikia Juni 5.


No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...