Search This Blog
Saturday, June 20, 2020
Simba na Mwadui kuvaana leo
LEO Uwanja wa Taifa, Simba itawakaribisha Mwadui FC kwenye mchezo wa Ligi Kuu Bara utakaochezwa majira ya saa 10:00 jioni.
Simba itashuka uwanjani ikiwa na kumbukumbu ya kulazimisha sare ya kufungana bao 1-1 na Ruvu Shooting Uwanja wa Taifa, Juni 14 huku Mwadui FC wakiwa wametoka kupoteza mchezo wao mbele ya Yanga kwa kufungwa bao 1-0 Uwanja wa Kambarage.
Kocha Mkuu wa Simba, Sven Vandenbroeck amesema kuwa wapo tayari kuvaana na Mwadui kwa kuwa makosa yao wameyafanyia kazi.
"Makosa ya mchezo wetu uliopita dhidi ya Ruvu Shooting tumeyafanyia kazi, tuna amini tutapata matokeo mbele ya Mwadui FC kwani malengo yetu ni kupata matokeo chanya," amesema.
David Chakala, Meneja Mkuu wa Mwadui FC amesema kuwa benchi la ufundi limejipanga kuona nao wanapata pointi tatu ili kujiweka kwenye nafasi nzuri.
Simba ipo nafasi ya kwanza ikiwa na pointi 72 huku Mwadui FC ikiwa nafasi ya 12 ikiwa na pointi 34 zote zimecheza mechi 29.
Kwenye mchezo wa kwanza uliochezwa Uwanja wa Kambarage Simba ilinyooshwa bao 1-0 zama zile ikiwa chini ya Patrick Aussems.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...
No comments:
Post a Comment