Search This Blog

Saturday, June 27, 2020

Siku ya Kupiga vita dawa za kulevya


Wakati Tanzania ikiadhimisha siku ya kimataifa ya kupiga vita dawa za Kulevya, kwa kipindi cha takribani miaka mitano Tanzania imefanikiwa kupunguza uingizwaji wa dawa za kulevya kwa asilimia 90 huku zaidi ya watuhumiwa elfu 70 wakikamatwa.

Akizungumizia maadhimisho hayo na mafanikio yaliyopatikana Waziri wa nchi ofisi ya waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na wenye ulemavu Jenista Mhagama anasema mafanikio hayo yamepatikana baada ya kubaini na kuvunja mitandao hiyo hapa nchini kwa kushirikiana na taasisi mbalimbali za kimataifa.

Pamoja na kazi hiyo iliyofanywa na serikali kwa kushirikiana nan chi mbalimbali na taasisi za kimataifa ili kudhibiti uingizwaji wa dawa hizo hapa nchini bado Dawa zinazozalishwa hapa nchini zinaonekana kuwa changamoto.

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...