Search This Blog
Thursday, June 4, 2020
Profesa Mgaya: Mwarobaini si salama kwa kujifukiza
TANGU kuingia kwa ugonjwa wa Covid- 19 ulioanzia nchini China, Desemba mwaka jana, watafiti mbalimbali duniani wameendelea kufanya tafiti ili kubaini dawa au kinga ya ugonjwa huo.
Miongoni mwa tafiti zinazoendelea ni pamoja na zile zinazofanywa hapa nchini, ikiwamo inayofanywa na Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR).
HISTORIA YA NIMR
Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya NIMR, Profesa Yunus Mgaya, anasema kuwa taasisi hiyo ilianzishwa kwa sheria ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, namba 23 ya mwaka 1979 na kuanza kufanya kazi rasmi mwaka 1980, ikiwa na wafanyakazi wanasayansi 13 sasa wameongezeka na kufikia 400.
NIMR ni taasisi iliyo chini ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, huku kazi yake kubwa ikiwa ni pamoja na kufanya utafiti, inaratibu, inakuza na kusimamia tafiti za afya zinazofanyika nchini na kukuza matumizi ya matokeo ya tafiti hizo.
Hadi sasa, ina idara ya tafiti za Tiba Asili ambayo jukumu lake ni kufanya utafiti juu ya dawa za miti shamba, ambazo nyingine zimekuwa zinatumika miaka mingi tangu enzi za bibi na babu zetu.
LENGO LA NIMR
Ni kuondoa mzigo wa magonjwa hasa yasiyopewa kipaumbele, pia kushirikiana na Serikali kufanya tafiti za kisayansi za afya na kuziratibu.
Kufanya udhibiti na tafiti za tiba za asili na kushauri serikali au Wizara ya Afya kwenye tafiti zinazofanyika na zina matokeo ya kisera hupeleka wizarani ili izitumie katika afua mbalimbali, utungaji sera na miongozo ya kitiba.
“Tunashukuru Mungu hadi sasa tuna miaka 40 katika utendaji kazi wetu lakini kuna tafiti 100 zinaendelea na nyingine tulizofanya zimeleta matokea mazuri katika jamii,” anasema Profesa Mgaya.
MATOKEO YA TAFITI
Akitolea mfano wa teknolojia ya uwekaji dawa kwenye vyandarua ulizinduliwa na taasisi hiyo, Amani mkoani Tanga.
Anasema pia usugu wa dawa ya malaria ya Chloroquine ni matokeo ya taasisi hiyo ambapo ilifanya utafiti kwa watu wengi na kubaini watu 10 wanaotumia dawa hiyo hawaponi.
Mgaya anasema pia amefanya tafiti mbalimbali kwenye magonjwa ya Kifua Kikuu, vimelea vya Ukimwi na magonjwa yasiyoambukiza.
“NIMR imedhamiria kupunguza vifo kwa wagonjwa wenye maambukizi ya fangasi (Cryptococcus Neofroman) na kusababisha homa ya UTI ya mgongo (Cryptococcal Meningitis) kwa wagonjwa walioathirika na Ukimwi,” anasema Profesa Mgaya.
Anasema utafiti wao wa awali walibaini kuwa kati ya watu 10 wenye Ukimwi wakipata fangasi wa UTI ya mgongo saba hufariki.
“Yaani katika watu 10 wakipata ugonjwa huu, asilimia 70 walikuwa wanakufa, lakini sasa hivi dawa hizi zimesaidia kupambana na virusi hivyo vya homa ya UTI wa mgongo,” anasema Profesa Mgaya.
Anasema waligundua mchanganyiko wa dawa mbili ambazo zinatolewa kwa sasa, zinazosaidia mgonjwa wa Ukimwi wakipata fangasi wapone. “Sasa hivi tumetoka asilimia 70 ya awali hadi kufikia 30, ambapo ilibainika baada ya kufanyika utafiti na miongozo ikatolewa,” anasema.
Anasema pia wanaendelea na tafiti za tiba nyingine ikiwamo zile zinazoikabili jamii ya watu wenye kipato cha chini mfano matende, mabusha, usubi na vikope.
MAFANIKIO
Mgaya anasema hadi sasa, NIMR imefanikiwa kuzalisha dawa mbalimbali ikiwamo ya tezi dume, seli mundu, malaria na dawa lishe ya NIMRCAF inayotumika kuimarisha kinga ya mwili.
Anasema bado wanaendelea na tafiti 100 ambazo zipo kwenye hatua mbalimbali.
Akizungumzia mchango wa NIMR katika kupambana na virusi vya corona, anasema walibaini dawa lishe ya NIMRCAF itokanayo na viungo asilia na kuleta matokeo bora katika kutibu dalili za awali za ugonjwa hatari wa COVID-19.
UTENGENEZAJI
Anasema dawa hiyo inatengenezwa kwa kufuata vipimo maalum kulingana na wingi wake, ambapo mchanganyiko wake unajumuisha tangawizi, pilipili kichaa, kitunguu maji chekundu, kitunguu swaumu na limao la kijani.
Anasema unaweza kutengeneza dawa hiyo kwa kutumia tangawizi punje tano, kitunguu maji kimoja, punje za kitunguu swaumu kumi, malimao mawili na pilipili kichaa ambapo unakatakata na kuzisaga pamoja kwenye mashine ya kusagia, kisha unaichuja na kuchanganya na maji nusu lita.
“Dawa hii kwa sasa ipo kwenye utafiti ili iweze kutoa ushuhuda wa kile kinachosemwa kama ina uwezo wa kutibu dalili za ugonjwa huo,” anasema Mgaya.
Akitolea mfano wa teknolojia ya uwekaji dawa kwenye vyandarua ulizinduliwa na taasisi hiyo, Amani mkoani Tanga.
Anasema pia usugu wa dawa ya malaria ya Chloroquine ni matokeo ya taasisi hiyo ambapo ilifanya utafiti kwa watu wengi na kubaini watu 10 wanaotumia dawa hiyo hawaponi.
Mgaya anasema pia amefanya tafiti mbalimbali kwenye magonjwa ya Kifua Kikuu, vimelea vya Ukimwi na magonjwa yasiyoambukiza.
“NIMR imedhamiria kupunguza vifo kwa wagonjwa wenye maambukizi ya fangasi (Cryptococcus Neofroman) na kusababisha homa ya UTI ya mgongo (Cryptococcal Meningitis) kwa wagonjwa walioathirika na Ukimwi,” anasema Profesa Mgaya.
Anasema utafiti wao wa awali walibaini kuwa kati ya watu 10 wenye Ukimwi wakipata fangasi wa UTI ya mgongo saba hufariki.
“Yaani katika watu 10 wakipata ugonjwa huu, asilimia 70 walikuwa wanakufa, lakini sasa hivi dawa hizi zimesaidia kupambana na virusi hivyo vya homa ya UTI wa mgongo,” anasema Profesa Mgaya.
Anasema waligundua mchanganyiko wa dawa mbili ambazo zinatolewa kwa sasa, zinazosaidia mgonjwa wa Ukimwi wakipata fangasi wapone. “Sasa hivi tumetoka asilimia 70 ya awali hadi kufikia 30, ambapo ilibainika baada ya kufanyika utafiti na miongozo ikatolewa,” anasema.
Anasema pia wanaendelea na tafiti za tiba nyingine ikiwamo zile zinazoikabili jamii ya watu wenye kipato cha chini mfano matende, mabusha, usubi na vikope.
MAFANIKIO
Mgaya anasema hadi sasa, NIMR imefanikiwa kuzalisha dawa mbalimbali ikiwamo ya tezi dume, seli mundu, malaria na dawa lishe ya NIMRCAF inayotumika kuimarisha kinga ya mwili.
Anasema bado wanaendelea na tafiti 100 ambazo zipo kwenye hatua mbalimbali.
Akizungumzia mchango wa NIMR katika kupambana na virusi vya corona, anasema walibaini dawa lishe ya NIMRCAF itokanayo na viungo asilia na kuleta matokeo bora katika kutibu dalili za awali za ugonjwa hatari wa COVID-19.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...


No comments:
Post a Comment