Makamu wa Rais wa Marekani Mike Pence ametangaza kufuta mikutano ya kampeni katika majimbo mawili ya Florida na Arizona iliyopangwa kufanyika wiki inayokuja baada ya majimbo hayo kushuhudia wimbi la visa vipya vya maambukizi ya virusi vya corona.
Pence alipangiwa kuwa na mkutano wa kampeni mjini Tuscan, Arizona siku ya Jumanne kabla ya kwenda Florida siku ya Alhamisi kwa mkutano mwingine kuelekea uchaguzi mkuu wa mwezi Novemba.
Akizungumza akiwa mjini Washington, Pence amesema amefuta ratiba hiyo na badala yake atayatembelea majimbo hayo mawili pamoja na Texas kupata taarifa za kina juu ya kuongezeka kwa visa vya ugonjwa wa COVID-19 kwenye maeneo hayo.
Magavana wa majimbo hayo matatu wanakabiliwa na ukosoaji mkubwa wa kuendelea na mipango ya kufungua tena shughuli za kawaida licha ya kuongeza kwa visa vya maambukizi kwenye maeneo hayo.
Search This Blog
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment