Search This Blog
Sunday, June 14, 2020
Kangi Lugola 'Rais Magufuli Amekuwa Kama Yesu Kristo Watanzania Wanamlilia na Kumfuata"
Mbunge wa Mwibara kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) Kangi Lugola, amesema kuwa watu kama Rais Magufuli hauwezi ukawapata popote pale na ndiyo maana hata alipoamua kumtengua kwenye nafasi yake ya Uwaziri alimshukuru na hivyo kumfananisha na Yesu Kristo.
Lugola ameyabainisha hayo leo Juni 13, 2020, Bungeni Dodoma wakati akichangia hoja ya Bajeti katika Mkutano wa 19, Kikao cha 45.
"Rais Magufuli amekuwa kama Yesu Kristo, Watanzania wanamlilia na kumfuata na ndiyo maana hata aliponitengua nilisema, ulinipa heshima ya huu Uwaziri na leo umetwaa Uwaziri ulio wako, jina la Magufuli libarikiwe, tunapokuwa na Rais kama huyu hatutakiwi kuingia kwenye mijadala ya kumtafuta mwingine" amesema Kangi Lugola.
Aidha Kangi ameongeza kuwa "Niliwahi kusema watu wa namna kama ya Rais Magufuli hawazaliwi kila wakati na hauwezi kuwapata kila mahala, watu ambao unaweza kuwapata kila mahala ni walevi kama kina Mbowe na habari ya mjini sasa hivi ni alilewa na kuvunjika mguu, na Rais Magufuli ninamfananisha kama Mwenge wa Uhuru".
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment