Search This Blog
Wednesday, June 3, 2020
Diamond ampoteza Davido
KIONGOZI wa lebo ya WCB, Naseeb Abdul maarufu kwa jina la Diamond Platnumz ameweka historia nyingine baada ya kutajwa kuwa msanii namba mbili kwa mafanikio Afrika kupitia mtandao wa Youtube.
Kwa mujibu wa Jarida la Billboard nchini Marekani, msanii huyo amekuwa mmoja kati ya wasanii wanaotumia vizuri mtandao wa Youtube kufanya mambo makubwa.
Msanii namba moja anayefanya vizuri kwenye mtandao huo ni Burna Boy kutoka Nigeria huku Diamond Platnumz akishika nafasi ya pili na nafasi ya tatu ikishikwa na Davido.
Meneja wa Youtube, Kevin Meenan ameeleza kushangazwa na mafanikio ya Diamonda ambaye ana wafuasi milioni 3.6 ambao ni sawa na asilimia 80 ya wanaotazama video zake wanatokea nje ya Tanzania.
Baada ya kupata taarifa hiyo Diamond alitumia kurasa zake za mitandao ya kijamii na kusema ‘Kufanya kazi kwa bidii, kusali na kujiamini ndio siri iliyojificha nyuma yake.’
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment