thabit madai
SHIRIKISHO la Soka visiwa Zanzibar (ZFF), limesema kwamba lipo tayari kuendelea na ligi kuu na ligi za madaraja yote za msimu wa mwaka 2019-2020 uliolazimika kusimamishwa kufuatia kuenea kwa Virusi vya Corona (COVID 19) Nchini.
Akitoa taarifa kwa vyombo vya Habari Mkurugenzi wa Mashindano wa Shirikisho hilo, Ali Mohamed Ali alisema kwamba ZFF imefikia hatua hiyo kutokana na agizo walilopatiwa na Shirikisho la mpira wa mguu barani afrika CAF kuwa hadi ifikapo May 5 wawe wameshatoa hatma za ligi za msimu wa mwaka 2019/2020.
"Leo tushawajibu CAF kwa barua kuwa ligi zote za madaraja zitaendelea ikiwa hali itaruhusu, nafikiri ligi za Madaraja ya Vijana hazitoendelea tena, kwaiyo CAF tumewajibu ligi yetu imesimama ikiwa hali itaruhusu tutaendelea, hapa kubwa tunasubiri zuio la serikali tu, wakiruhusu shughuli ziendelee, na muda ikiwa upo tutacheza tu, alobakisha mechi 8 atacheza 8, alobakisha 5 atacheza 5". Ali Muhammed Mkurugenzi wa Mashindano ZFF.
Search This Blog
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment