Search This Blog
Friday, May 22, 2020
WHO: Corona Haitaisha Leo, Safari Bado Ndefu
Mkurugenzi wa Shirika la Afya Duniani (WHO), Dkt. Tedros Adhanom Ghebreyesus amesema kumalizika kwa mlipuko wa Virusi vya Corona bado ni safari ndefu kufuatia ongezeko la maambukizi duniani.
Kauli yake inakuja baada ya Idadi kubwa zaidi kurekodiwa kwa siku moja tangu kuanza kwa mlipuko wa Corona, amabpo visa 106,000 vimeripotiwa katika Shirika hilo ndani ya saa 24 zilizopita.
Dkt. Tedros ameweka wazi wasiwasi uliopo kuhusu ongezeko la maambukizi kwenye nchi masikini na zenye uchumi wa kati. Aidha, Wataalamu wameonya kuwa idadi halisi ya maambukizi inaweza kuwa kubwa zaidi.
Hadi kufika sasa takribani Visa 5,129,453 vya wagonjwa wa covid -19 vimerekodiwa ulimwenguni, Wagonjwa 2,044,614 wamepona na 331,021 wamepoteza maisha.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment