Chama cha Waandishiwa Habari Wanawake Tanzania, Zanzibar (TAMWA, ZNZ) kinawatakia waislam wote sikukuu njema ya Mfunguo Mosi baada ya kufunga mwezi mtukufu wa Ramadhani.
Tunaelewa siku hiyo ni siku ya furaha kwa waislam wote nchini husherehekea kwa mipango mbali mbali ikiwemo kuwavisha nguo nzuri watoto wao kwenda kusalimia ndugu na jamaa.
Tunapenda pia kuchukuwa nafasi hii kuwatahadharisha wazazi kuwa karibu sana na watoto wao wakati wa sikukuu ili kujikinga na vitendo vya udhalilishaji.
Katika miaka iliyopita kipindi cha sikukuu huripotiwa kesi nyingi za udhalilishaji kwa wastani wa kesi tano kwa siku ambapo watoto waliopo chini ya umri wa miaka 18 hutoroshwa ama kubakwa.
Pamoja na kuwepo kwa janga la (COVID 19) ambapo kwa mwaka huu sikukuu haitakuwepo rasmi lakini tunaishauri jamii kuwadhibiti watoto ili kuepukana na vitendo hivi viovu ambapo wahalifu hupata fursa kutumia kipindi hichi cha kumalizika kwa mwezi mtukufu wa Ramadhani kufanya vitendo vyao viovu.
Baadhi ya watoto huonekana wakizurura kwa wingi maarufu kwenda kupokea mkono wa Iddi na hivyo kuhatarisha ustawi wao ambapo wakati mwengine hugonga hata kwenye nyumba wasizokuwa na mahusiano nazo.
Mara nyengine huingia katika nyumba ambazo wanaishi wabakaji na hivyo kuwafanyia vitendo vibaya na pia hata mtaani hurubuniwa kwa kuambiwa wakapewe sikukuu yao.
Hivyo, ni vyema watoto kubakia chini ya uangalizi wa wazee wao kwa wakati wote; mchana na jioni ili kujilinda kutokana na wabakaji lakini pia dhidi ya maradhi ya corona.
Tunapenda pia kuwakumbusha wananchi kujilinda na maradhi ya corona kwa vile yanaweza kuepukika pindi tukifata maagizo ya wataalamu.
Search This Blog
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment