Search This Blog
Thursday, May 21, 2020
RC Zambi amtaka DED wa halmashauri ya Kilwa awachukulie hatua kali watumishi wa kituo cha afya
Na Ahmad Mmow, Lindi.
Mkuu wa mkoa wa Lindi, Godfrey Zambi amemtaka mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya Kilwa, Renatus Mchau awachukulie hatua kali za kinidhamu baadhi ya watumishi wa kituo cha afya cha Pande ambao wamekopeshana fedha zilizokusanywa na kituo hicho.
Zambi alitoa agizo hilo katika kikao cha baraza la madiwani la halmashauri ya wilaya ya Kilwa baada ya kubaini watumishi hao wamekopeshana fedha zilizokusanywa na kituo hicho kwa ajili ya kununulia dawa na matumizi mengine ya kituo hicho.
Alisema nijambo lisilokubalika kuona fedha hizo zinatumika vibaya huku zikitakiwa kutumika kwa maslahi mapana ya umma.¥ Alisema tabia ya kutumia fedha vibaya inasababisha upungufu wa dawa kwenye vituo vya afya na zahanati.
Hivyo kusababisha wananchi kukosa huduma kwenye vituo hivyo vya kutolea huduma za afya.
Zambi alibainisha kwamba kituo hicho utendaji wake hauridhishi. Huku akiweka wazi kwamba asilimia 50 ya fedha zinazokusanywa zinatakiwa kununulia dawa.
Hata hivyo baadhi ya zahanati, vituo vya afya na hospitali hazitekelezi sharti hilo. Badala yake wanatumia chini ya asilimia 50 ya fedha zinazokusanywa.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment