Search This Blog
Saturday, May 9, 2020
Picha za Ngono zavuruga Vikao vya Bunge kwa Muda
Hili jambo lingetokea Bongo sijui ingewaje najaribu kuwaza tu kwakuwa mabunge mengi likiwemo la Tanzania hivi sasa linatumia teknolojia Zaidi katika kuendesha vikao vyake.
Imeelezwa kuwa huko Afrika kusini ambako wanendelea na lockdowan kufuatia janga la ugonjwa wa corona mkutano wa Bunge la nchi uliokuwa ukifanyika kwa njia ya mtandao umevurugika baada ya wadukuzi kutupia picha za utupu.
Asubuhi ya jana Mei 7, 2020 picha za ngono zilitokea katika skrini za wana mkutano huku sauti ya mwanamume ikisikika kumtusi Spika Thandi Modise, ambaye alikuwa mwenyekiti wa kikao hicho.
South Africa Parliament Video Call Hacked With Pornography | TimeSpika huyo aliyeshikwa na hasira alipaza sauti akisema hiyo ndio sababu anapinga mikutano ya mitandaoni.
“Hiki kilichotokea ni kilekile nilichokuwa ninakisema kuhusu kufanya mikutano kwa njia ya ‘Zoom’ Modise amenukuliwa akisema hivyo na tovuti ya Times Live.
Wabunge walielezea tukio hilo kama lenye kukera na kutatiza akili, kulingana na Tovuti ya habari ya Eyewitness.
Hali hiyo Iliwalazimu wataalamu wa Bunge kutuma kiunganishi chengine ambapo wabunge waliunganika tena na kuendelea na kikao chao.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment