Search This Blog
Monday, May 25, 2020
Naibu waziri Kanyasu akerwa na Wavamizi Mapito ya wanyamapori
Na John Walter-Manyara
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Constantine Kanyasu amekerwa na wananchi wanaojenga nyumba na kuendesha shughuli za kilimo katika maeneo yenye wanyamapori hasa katika mapito ya wanyamapori katika eneo la Kwakunchinja linalounganisha Hifadhi ya Taifa ya Tarangire na Hifadhi ya Manyara.
Amesema kutokana na tabia hiyo, serikali haiwezi kumaliza kulipa vifuta jasho na vifuta machozi kwa wananchi wanaoshambuliwa na wanyamapori wakali na waharibifu.
Akizungumza na viongozi wa Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori ya Burunge (WMA) Wilaya ya Babati mkoani Manyara, amesema ni vyema sasa Viongozi hao kutafakari na kuona namna ya kulinda ushoroba wa eneo la Kwakunchinja ambao ni muhimu kwa wanyamapori wanaotoka Hifadhi ya Taifa ya Tarangire kuelekea Hifadhi ya Ziwa Manyara.
Ameeleza kuwa, mwaka 2020 pekee, serikali imetumia Shilingi bilioni moja katika kulipa vifuta jasho na vifuta machozi kwa wananchi huku Sh bilioni 2.3 zikiwa hazijalipwa kwa wananchi walioathiriwa na wanyamapori wakali na waharibifu.
Kanyasu amesema kila mahali wananchi wamekuwa wakilalamika kuchelewa kulipwa vifuta jasho na vifuta machozi kutokana na madai hayo kuwa mengi hali inayosababisha wizara kuwa na madai mengi yasiyolipika kutoka kwa wananchi ambao baadhi wameyafuata makazi ya wanyamapori.
Amesema serikali inatafuta mbinu mbadala ya kupunguza migogoro baina ya binadamu na wanyamapori wakali na waharibifu baada ya kugundua fidia sio suluhisho kutokana na wimbi kubwa la wananchi kuendesha shughuli za kibinadamu shoroba za wanyamapori na maeneo ya mitawanyiko ya wanyamapori.
Amesema kutokana na baadhi ya wananchi kufanya makazi maeneo hayo, wizara imegundua hata ikitenga bajeti nzima ya wizara kwa ajili ya kulipa vifuta jasho na vifuta machozi haitaweza kumaliza tatizo hilo.
Alisema binadamu wamekuwa wakiwafuata wanyamapori hivyo suala la mazao ya kushambuliwa ni jambo lisiloepukika.
“Sehemu ya Mapori ya Akiba na Jumuiya ya Hifadhi za Wanyamapori ndimo wananchi wameanzisha makazi hivi unategemea wanyamapori watulie tu,” alihoji Kanyasu.
Aidha ameshauri kuwekwa Kamera,mabango yanayohimiza madaerava kuendesha mwendo wa taratibu na kuanisha faini zinazopasa kutozwa kwa atakaeua Mnyama wakati akiendesha maeneo ya hifadhi.
Amemtaka Mkuu wa wilaya ya Babati, Elizabeth Kitundu kuhakikisha anawatumia watendaji wa vijiji vilivyoko jirani na hifadhi kuhakikisha wanazuia uuzaji maeneo ya mapitio ya wanyamapori kwa wananchi.
Mkuu wa wilaya ya Babati Elizabeth Kitundu, akifunga kikao hicho muhimu alimuahidi Naibu waziri kuwa amepokea maagizo hayo na kinachofuata ni utekelezaji ili kuhakikisha rasilimali hiyo muhimu ya Wanyamapori inaendelea kuwepo katika hifadhi hizo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...
No comments:
Post a Comment