Search This Blog
Sunday, May 10, 2020
Mkuu wa zamani wa polisi ajiunga na kundi la Taliban
Mkuu wa zamani wa polisi amejiunga na kundi la Taliban katika mkoa wa Magharibi wa Farah, wizara ya mambo ya ndani ya Afghanistan imesema.
Taarifa ya wizara hiyo imesema kuwa Meja jenerali Abdul Jalil Bakhtwar ambaye aliwahi kuwa mkuu wa polisi katika mkoa wa Farah kati ya mwaka 2002 hadi 2004, amejiunga na wanamgambo hao wanaoipinga serikali ya mjini Kabul.
Wizara hiyo imeonyesha kusikitishwa na hatua ya afisa huyo kujiunga na Taliban ikisema amejiunga na maadui wa watu wa Afghanistan.Kundi la Taliban limethibitisha kuwa Bakhtwar amejiunga nao pamoja na watu wengine na kuwa amekaribishwa vizuri.
Akizungumza na shirika la habari la DPA mwanawe Bakhtwar, Masoud Bakhtwar ambaye ni naibu gavana wa mkoa wa Farah amekanusha vikali kuwa babake amejiunga na Taliban.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment