Mbunge wa Kilombero kwa tiketi ya chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA Peter Lijualikali amelieleza Bunge kuwa uamuzi wa kiongozi wa kambi rasmi ya upinzani Bungeni Freeman Mbowe kuwa wabunge wote wa chama hicho wajiweke karantini kwa siku 14 hayakuwa makubaliano ya wabunge bali amri ya kiongozi huyo uamuzi ambao hakukubaliana nao tangu awali.
Akiwa analia kwa uchungu Lijuakali alisema "Mheshimiwa spika mimi niliingia bungeni lakini sijalala siku mbili kwasababu ya maumivu, mimi nimelala jera miezi sita kwasababu ya CHADEMA kwasababu ya chama changu leo natekeleza wajibu wangu naambiwa ni kwasababu ya posho mh. spika nimeumiatunalilia katiba mpya ya nchi wakati ya kwetu ya CHADEMA TUNAIVUNJA"
"Kiuhalisia uamuzi wa kuambiwa tusije bungeni haukuwa wa kidemokrasia wala hapakuwa na makubaliano yoyote palikuwa na amri. Watu wanaambiwa tumefuata posho wakati nimekuja kufanya kazi yangu ya kibunge. Mimi nimekaa jela miezi sita kwa sababu ya CHADEMA na imani yangu kwenye chama, leo nakuja kutimiza wajibu wangu naambiwa sababu ya posho"
Search This Blog
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment