Search This Blog
Saturday, May 2, 2020
Klabu za ligi ya Uingereza kujadiliana kuhusu uwezekano wa kurejea viwanjani
Klabu katika ligi kuu ya Uingereza zinatarajiwa kufanya mazungumzo leo kuhusu namna ya kumaliza msimu. Haya yanajiri huku mshambulizi wa Manchester City, Sergio Aguero, akikiri kuwa wachezaji wana wasiwasi kwamba wanaweza kuharakishwa kurudi viwanjani.
Ligi hiyo ya Uingereza inakabiliwa na kitisho cha kupata hasara ya euro bilioni moja ikiwa mechi hazitachezwa tena kwa sababu ya janga la corona.
Suluhisho la hasara hiyo ni kuzicheza jumla ya mechi 92 ambazo zimesalia hata bila ya kuwepo mashabiki uwanjani.
Lakini ligi hiyo inakumbwa na changamoto nyingi za kimkakati katika majaribio yake kutaka kurejea viwanjani mnamo wakati Uingereza ikiwa kati ya mataifa yaliyoathiriwa mno na janga la COVID-19.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment