Search This Blog

Friday, May 1, 2020

Kim Jong-un Aonekana Hadharani, Afanya Hili Kukiwa na Tetesi Kuwa Amefariki



Kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Jong-un ameonekana hadharani kwa mara ya kwanza, kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Shirika la Habari la nchi hiyo ‘KCNA’ leo, Mei 2, 2020, wakati ambapo kuna uvumi kuwa huenda alikuwa mahututi au amefariki dunia.

Taarifa hiyo imeeleza kuwa Kim amekata utepe na kufungua kiwanda kikubwa cha mbolea katika mji mkuu wa chi hiyo, Pyongyang, tukio lililofanyika Ijumaa, Mei Mosi, 2020.

KCNA imeripoti kuwa tukio hilo lilihudhuriwa na watu wengi ambao waliitikia kwa shangwe kuu baada ya kiongozi huyo kukata utepe kuashiria kufunguliwa kwa kiwanda hicho.

Imeelezwa kuwa aliongozana na maafisa waandamizi wa serikali akiwemo mdogo wake, Kim Yo Jong.

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...