Search This Blog
Tuesday, May 12, 2020
India Nayo Yashtuka Kuhusu CORONA...Yarudisha Usafiri wa Treni Kwa Tahadhari
Usafiri wa reli nchini India ni muhimu sana ambapo kwa siku, abiria zaidi ya milioni 20 hutumia usafiri huo, leo Serikali imetangaza kufungua tena huduma ya usafiri wa reli na itaendesha treni chache.
Treni maalumu zitaanza kufanya tena kazi katika majiji makubwa ikiwemo New Delhi na Mumbai, wakati nchi hiyo ikianza kulegeza vizuizi vyake vya karibu wiki saba, wakati maambukizi ya virusi vya corona yakiongezeka.
Abiria wataruhusiwa kuingia kwenye vituo vya treni baada ya kupimwa joto la mwili, kuheshimu umbali kati ya mtu na mtu na kupewa dawa za kujitakasa mikono.
Usafiri wa reli, barabara na anga ulisitishwa mwishoni mwa mwezi Machi kama sehemu ya hatua kali za nchi nzima za kukabiliana na covid-19.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment