Search This Blog
Monday, May 18, 2020
China yatoa radiamali kuhusu kifo cha balozi wake huko Israel
Gazeti moja la China limeandika kwamba, kifo cha balozi wa nchi hiyo katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu (Israel) kilitokea baada ya yeye kukosoa siasa chafu za kupenda kujitanua za Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Mike Pompeo.
Gazeti la South China Morning Post limeinukuu Wizara ya Mambo ya Nje ya China ikisema kuwa Du Wei (57) balozi wa nchi hiyo huko Tel Aviv, mji mkuu wa utawala haramu wa Kizayuni amefariki dunia katika hali isiyo ya kawaida. Limeongeza kwamba Beijing itatuma wataalamu wake kuchunguza sababu za kifo cha mwanadiplomasia huyo na pia kuusafirisha mwili wake. Hii ni katika hali ambayo polisi wa utawala bandia wa Israel walikuwa wamejizuia kutangaza sababu za kifo cha balozi huyo wa China.
Kanali ya televisheni ya 12 ya utawala wa Kizayuni imetangaza kwamba Du Wei alifariki dunia katika hali ya kawaida akiwa usingizini nyumbani kwake. Hivi karibuni, Mike Pompeo, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani aliikosoa vikali serikali ya China akiituhumu kuwa inahusika na kuenea kwa virusi vya Corona duniani, huku kwa upande wake serikali ya Beijing ikiituhumu Marekani kuwa chanzo kikuu cha virusi hivyo nchini China na katika mataifa mengine ya dunia.
Siku chache zilizopita gazeti la Jerusalem Post la Israel lilichapisha taarifa iliyotolewa na Bwana Du Wei akimkosoa vikali Mike Pompeo na siasa za Marekani za kupenda kujitanua.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...


No comments:
Post a Comment