WANAFAMILIA wa Yanga ambao ni mabosi pia Kampuni ya GSM imesema kuwa iwapo kuna klabu ndani ya Bongo ama nje ya nchi itahitaji saini ya nahodha Papy Tshishimbi inapaswa isubiri mpaka mkataba umalizike.
Maneno hayo ni ujumbe kwa watani wao Simba ambao ilielezwa kuwa wanahitaji saini ya nyota huyo ili akaongeze makali ndani ya kikosi cha Simba.
Mkurugenzi wa Uwekezaji ndani ya GSM Injinia Hersi Said amesema:"Kuhusu kapteni Tshishimbi yeye ni mchezaji muhimu na tumemalizana naye ambapo dili limekamilika na yeye mwenyewe amekubali kwa kusema 'dealdone'.
"Kwa wale ambao wanahitaji kuipata saini yake basi inawabidi wasubiri mpaka pale mkataba utakapoisha ili waweze kuipata saini yake ila kwa sasa atabaki ndani ya Yanga,".
Inaelezwa kuwa mkataba wa Tshishimbi ambao ulikuwa unameguka mwezi wa nane umeboreshwa kwenye upande wa maslahi jambo ambalo limemfanya akubali kusaini.
Search This Blog
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment