Search This Blog

Thursday, April 16, 2020

WHO laipongeza Uturuki


Shirika la Afya la Umoja wa Mataifa lapongeza Uturuki kwa kutoa msaada katika  jitihada za kkupamana na Covid-19.
 
Shirika la Afya la Umoja wa Mataifa WHO laipongeza Uturuki kwa kutoa msaada  katika mataifa tofauti katika juhudi za kupamabana na  virusi vya corona.

Hans Kluge amesema kuwa nafahamu kile kinachofanya na Uturuki katika juhudi za kupambana na virusi vya corona.

Uturuki inatoa msaada wa vifaa vya matibabu na madawa  kwa mataifa tofauti amesema Hans Kluge.
Kluge ameendelea kufahamisha kuwa  msaada kutoka Uturuki  kuelekea Uingereza, Italia, Uhispania na mataifa ya Balkans  na jambo linalohitaji kupongezwa kwa kuwa malengo yake ni kuzuia maambukizi ya virusi vya corona.

Mkurugenzi wa shirika la Afya la Umoja wa Mataifa katika  eneo hilo amesema kwamba kitend hicho cha Uturuki ni cha kibinadamu.

Akijibu moja ya maswali kutoka kwa wanahabari, Kluge amesema kwamba Uturuki imetoa msaada wa vifaa vya matibabu na madawa  kwa kiasi kikubwa kwa mataifa ya Ulaya kuliko mataifa mengine ulimwenguni.

Mkutano huo kati ya Kluge na wanahabari umefanyika kwa njia ya video, mkutano ambao suala zima kuhusu virusi vya corona na mbinu za kukabiliana navyo limejadiliwa.


No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...