Search This Blog

Sunday, April 5, 2020

Ugonjwa wa Corona Wamtia Simanzi Mbwana Samatta


Nahodha wa timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars anayecheza soka la kulipwa katika club ya Aston Villa ya England Mbwana Samatta ameonekana kuwa miongoni mwa watu wanaopata mawazo sana wakati huu wa virusi vya corona.

“Haya maisha ya kuwa tu ndani yamenifanya niwafikirie zaidi wenzetu waliopo magerezani… nina uhuru wa kwenda supermarket na wa kula chakula ninachokitaka achana na tv, simu, kitanda chenye joto😁(if you know what I mean) wenzetu hawana hivi vitu..tuwaombee sana wanayopitia ni magumu”>>> Samatta

Samatta amejiunga na Aston Villa Janury 2020 akisaini mkataba wa miaka minne na nusu akitokea KRC Genk ya Ubelgiji hadi sasa amecheza game 6 na kufunga magoli 2 kabla ya Ligi kusimama.

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...