Search This Blog

Sunday, April 5, 2020

Trump Awataka Wamarekani kujiandaa kwa idadi ya kutisha sana ya vifo vya Corona

Rais wa Marekani Donald Trump amewaonya Wamarekani kujiandaa kwa idadi ya kutisha sana ya vifo kutokana na virusi vya corona katika siku chache zijazo. 

Trump amesema Marekani inaingia katika kipindi ambacho idadi ya vifo itapanda kwa kasi. 

Hata hivyo, Rais huyo amesema Marekani haiwezi kuendelea kusitisha shughuli zake milele akiongeza kuwa itafika wakati ambao maamuzi magumu yatafanywa.

 Wakati visa vya maambukizi ya COVID-19 nchini Marekani vikithibitishwa kupindukia 300,000 kukiwa na zaidi ya vifo 8,300, kuna habari za kutia moyo nchini Italia na Uhispania ambako idadi ya imeanza kupungua. 

Sasa kuna visa milioni 1.17 vya maambukizi vilivyothibitishwa kote duniani na kumekuwa na vifo 63, 437 tangu mlipuko wa virusi hivyo ulipoanza nchini China mwaka jana. 

DW


No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...