Search This Blog
Sunday, April 12, 2020
Raia wa China Kufikishwa Mahakamani Kwa Tuhuma za Kugoma Kunawa Mikono
Katavi. Jeshi la polisi Mkoa wa Katavi linatarajia kumfikisha mahakamani raia mmoja wa China Lin Guosong (34) mfanyabiashara wa Majengo Sumbawanga akituhumiwa kukiuka amri halali iliyowekwa na Serikali ya kunawa mikono kujikinga na corona.
Akizungumza na Mwananchi kwa njia ya simu leo Aprili 11,2020 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi, Benjamini Kuzaga amesema mtuhumiwa amekiuka utaratibu huo Aprili 5, 2020 katika kizuizi cha Ntibili Majimoto.
"Mtuhumiwa alikuwa anaendesha gari lenye namba za usajili... akiwa na msaidizi wake James Mpepo (28)mkazi wa Bomani Sumbawanga, baada ya kufika eneo hilo mwenzake alishuka na kutii amri ya kunawa lakini yeye alikaidi," amesema Kuzaga.
Kuzaga amesema Ofisa Mtendaji wa Kijiji cha Ntibili, Josephat Mgelwa alitoa taarifa kituo cha polisi Majimoto ambapo polisi walifika eneo hilo na kumkamata mtuhumiwa.
"Baada ya kumhoji hakuwa na maelezo yoyote, pia mwezake alimsihi kushuka ili anawe alikataa bila kuwa na sababu za msingi, polisi walichukua hati yake ya kusafiria Na.E09809632, na muda wowote tutamfikisha mahakamani baada ya sikukuu,"
Mwananchi
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment