Search This Blog

Sunday, April 5, 2020

Makonda kuanza kuwakamata wazururaji leo

Leo April 6, 2020, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda, ataanza rasmi zoezi la kuwakamata wazururaji wote wa Mkoa huo, wanaoingia mjini bila ya kuwa na kazi yoyote ikiwa ni tahadhari ya Virusi vya Corona.


Makonda amesema kuwa haina haja kwa mtu kuendelea kuzurura ili hali anatambua kabisa Dunia ipo kwenye wakati gani na hivyo mtu kama hana kitu cha msingi cha kufanya ni bora abaki nyumbani.

"Umuhimu wa kuchapa kazi uko palepale, kuanzia Jumatatu tutakamata wazururaji wote mjini wasiokuwa na kazi ya maana, hao ndiyo wanaosababisha mikusanyiko isiyokuwa na tija, unaenda stendi, Sokoni, Bandarini huna kazi huo ni uzururaji unahatarisha maisha ya watu wengine" amesema Makonda.

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...