Search This Blog

Monday, April 13, 2020

Kesi ya pili ya kifo cha Ebola yaripotiwa katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo

Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imeripoti kesi ya pili ya kifo cha Ebola katika kipindi cha siku tatu baada ya nchi hiyo kupitia muda wa zaidi ya majuma sita bila ya kuripotiwa kesi mpya ya maambuzo ya Ebola.

Shirika la Afya Duniani (WHO) limetangaza habari hiyo na kueleza kwamba, aliyeaga dunia kwa Ebola ni binti wa miezi 11 ambaye anasadikiwa kuambukizwa na mgonjwa aliyeaga dunia kwa maradhi hayo Ijumaa ya juzi huko katika mji wa Beni.

Hayo yanaripotiwa katika hali ambayo, leo amhuri ya Kidemokrasia ya Congo ilitarajiwa kutangaza rasmi kumalizika kabisa ugonjwa huo katika nchi hiyo ambao umeua zaidi ya watu 2,200.


No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...