Search This Blog

Thursday, April 23, 2020

Eymael akata mzizi wa fitna kwa Metacha Mnata

By Thomas Ng’itu

Dar es Salaam. Kocha wa Yanga, Luc Eymael ameamua kukata mzizi wa fitna kwa makipa wake baada ya kuweka wazi siri ya kumpa nafasi Metacha Mnata katika kikosi chake.

Metacha aliyesajiliwa na Yanga msimu huu akitokea Mbao amekuwa na kiwango kikubwa mbele ya makipa wenzake, Faroukh Shikhalo na Ramadhani Kabwili.

Eymael aliliambia Mwananchi makipa wote wazuri lakini kiwango ambacho anakionyesha Metacha ndio kimemfanya apate nafasi mara kwa mara.

“Metacha yupo katika timu ya Taifa hilo kila mmoja analijua, tumekuwa na ratiba ngumu lakini bado anafanya vizuri,” alisema.

Kocha huyo alifunguka zaidi na kusema ni ngumu kubadili makipa wakati yupo ambaye ana kiwango cha kumvutia na anafanya vyema uwanjani.

Let's block ads! (Why?)

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...