Search This Blog
Thursday, April 23, 2020
Everton Yamuwinda Mbwana Samatta
Baba mzazi wa mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana Samatta, mzee Ally Samatta amefunguka kuwa anaamini mtoto wake ataendelea kucheza Ligi Kuu England hata ikitokea Aston Villa ikishuka daraja kwa kuwa tayari timu ya Everton imejipanga kumchukua.
Mshambuliaji huyo amejiunga na Villa kwa mkataba wa miaka minne na nusu katika kipindi cha dirisha dogo akitokea KRC Genk ya nchini Ubelgiji.
Mzee Samatta amesema kuwa kwa sasa mtoto wake anaendelea kufanya mazoezi binafsi kwa lengo la kutaka kuisaidia timu yake isishuke daraja lakini hata kama itatokea kushuka basi atajiunga na Everton kwa kuwa wameonyesha nia ya kutaka kumnunua ikiwa Aston Villa watashuka daraja.
“Samatta amekuwa akifanya mazoezi binafsi kwa sababu ya Corona na ukiangalia hata familia yake ipo kule baada ya kwenda kumtembelea, anachokiangalia kikubwa ni kuona Villa wanabaki katika Ligi Kuu England na wapo kwenye nafasi mbaya.
“Suala la kushuka thamani siyo ishu sana kwa sababu Everton wamekuwa kwenye mawindo ya kuweza kumnunua kama itatokea Villa wanashuka daraja,” alisema mzee Samatta.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment