Search This Blog
Sunday, April 5, 2020
Baada ya Mbunge Kukosa Hewa Wakati Anachangia, Spika Awatahadharisha Wabunge "Makombora ni Mengi Kuelekea Uchaguzi Kuweni Makini"
WAKATI Bunge likielekea ukingoni na wabunge kurudi tena kwenye Uchaguzi Mkuu mwaka huu 2020, Spika wa Bunge Job Ndugai amewashauuri wabunge hao kuwa makini kwani makombora ni mengi kipindi hiki.
Akizungumza leo Bungeni Mjini Dodoma Spika Ndugai amewaambia wabunge kuwa hiki ni kipindi ambacho wanatakiwa kuwa makini wakati huu wa kuelekea kwenye uchaguzi mkuu makombora jimboni yanakuwa mengi, hivyo wachukue tahadhari.
Ushauri huo wa Spika Ndugai kwa wabunge umekuja baada ya Mbunge Anastazia Wambura kushindwa kuendelea kuchangia Bungeni baada ya kueleza kuwa anakosa hewa na sauti inakauka."Mheshimiwa Spika naona nakosa hewa,"alikuwa akisikika mbunge huyo .Hata hivyo aliomba kuunga mkono hoja na kukaa kwenye kiti chake.
Baada ya kutoa maelezo hayo ,Spika Ndugai ndipo aliposikika akiwaambia wabunge wawe makini maana dakika zenyewe hizi ni za kuelekea uchaguzi mkuu , hivyo makombora ni mengi."Tena na hivi kuna Corona unaweza kukutana na kombora halafu wakasema Corona. Watani zangu wanyamwezi wanajua namna ya kujifusha ule moshi kwa kujifunika shuka, tuwe makini."
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment