Search This Blog
Wednesday, March 18, 2020
UDSM watoa saa 48 wanafunzi kuondoka
Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) nchini Tanzania kimewataka wanafunzi wote kuhakikisha ifikapo Ijumaa Machi 20, 2020 wawe wameondoka kurejea nyumbani.
UDSM imetoa taarifa hiyo leo Jumatano Machi 18,2020 ikiwa ni saa chache kupita tangu Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa atangaze kuvifunga vyuo vyote kutokana na kujikinga na virusi vya ugonjwa wa corona (CODIV-19).
Agizo hilo la Majaliwa amelitoa baada ya wagonjwa wawili zaidi raia wa kigeni kubainika kuwa na virusi vya corona wakiwa Dar es Salaam na Zanzibar hivyo kufikisha idadi ya waliobainika nchini humo kuwa watatu.
Katika taarifa ya Makamu mkuu wa UDSM, Profesa William Anangisye imesema katika kutekeleza maelekezo na ushauri wa Serikali kwa lengo la kudhibiti kuenea kwa ugonjwa huo, shughuli zote za masomo chuoni hapo zimesitishwa kuanzia leo Machi 20 2020 hadi hapo itakapotangazwa vinginevyo.
“Kutokana na masomo kusitishwa, wanafunzi wote, wa programu zote, walioko likizoni wanatakiwa kubaki nyumbani huko waliko, hadi hapo watakapotaarifiwa kurejea chuoni,” amesema Profesa Anangisye
Makamu mkuu huyo wa chuo amesema, “wanafunzi wote wa programu zote, ambao kwa sababu mbalimbali bado wapo katika kampasi yoyote ya chuo wanatakiwa kuwa wameondoka chuoni ifikapo Ijumaa Machi 20, 2020, kwenda nyumbani hadi hapo watakapotaarifiwa kuwa chuo kimefunguliwa tena.”
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment