Search This Blog

Wednesday, March 4, 2020

Serikali kupandisha kodi uingizwaji wa bidhaa za ngozi za mtumba nchini

Waziri wa viwanda na biashara nchini,Innocent Bashungwa amesema serikal inampango wa kupandisha kodi kwenye uingizwaji wa bidhaa za ngozi za mtumba nchini ili kuongeza thamani ya uzalishaji na utumiaji  wa bidhaa za ngozi hapa nchini

Waziri Bashungwa amesema hayo leo March 04.2020, wakati akitembelea kiwanda cha ngozi cha Himo Tanneries  L.T.D ambapo amesema ili kuongeza thamani hiyo watanzania wanapaswa kuwa wazalendo kwa kupenda na kutumia bidhaa zao asilia zinazozalishwa nchini kwa ikiwemo za ngozi kwa lengo la kuinua uchumi wao na raifa kwa ujumla.

"Serikali inaendelea kuhakikisha uchumi wa viwanda unaongezeka mara dufu kwa kuungwa mkono na wadau pamoja na watanzania wwnyewe,bidhaa hizi za ngozi ni nzuri sana na zinadumu kwanini tusiunge juhudi za  wazalishaji wa bidhaa hii ya ngozi hapa nchini,wanazalisha viatu,mikanda,mikoba mbalimbali"amesema Waziri Bashingwa.

Pia amesema atahakikisha shule zinaingia ubia na viwanda vya ngozi vilivyopo nchini ili kujenga utamaduni wa jamii ya watanzania wanaokua kutumia bidhaa za ngozi na kuinuka kiuchumi.

Kwa upande wake mkurugenzi wa kiwanda hicho cha ngozi cha Himo Tannaries,Sabas Herman Oisso ameiomba serikali kusaidia kuhamasisha watanzania juu ya umuhimu wa  kutumia bidhaa za ngozi zinazozalishwa hapa nchini badala ya kununua zinazozalishwa nje siziso na ubora wa kutosha tena zenye gharama kubwa.

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...