Waziri wa viwanda na biashara nchini,Innocent Bashungwa amesema serikal inampango wa kupandisha kodi kwenye uingizwaji wa bidhaa za ngozi za mtumba nchini ili kuongeza thamani ya uzalishaji na utumiaji wa bidhaa za ngozi hapa nchini
Waziri Bashungwa amesema hayo leo March 04.2020, wakati akitembelea kiwanda cha ngozi cha Himo Tanneries L.T.D ambapo amesema ili kuongeza thamani hiyo watanzania wanapaswa kuwa wazalendo kwa kupenda na kutumia bidhaa zao asilia zinazozalishwa nchini kwa ikiwemo za ngozi kwa lengo la kuinua uchumi wao na raifa kwa ujumla.
"Serikali inaendelea kuhakikisha uchumi wa viwanda unaongezeka mara dufu kwa kuungwa mkono na wadau pamoja na watanzania wwnyewe,bidhaa hizi za ngozi ni nzuri sana na zinadumu kwanini tusiunge juhudi za wazalishaji wa bidhaa hii ya ngozi hapa nchini,wanazalisha viatu,mikanda,mikoba mbalimbali"amesema Waziri Bashingwa.
Pia amesema atahakikisha shule zinaingia ubia na viwanda vya ngozi vilivyopo nchini ili kujenga utamaduni wa jamii ya watanzania wanaokua kutumia bidhaa za ngozi na kuinuka kiuchumi.
Kwa upande wake mkurugenzi wa kiwanda hicho cha ngozi cha Himo Tannaries,Sabas Herman Oisso ameiomba serikali kusaidia kuhamasisha watanzania juu ya umuhimu wa kutumia bidhaa za ngozi zinazozalishwa hapa nchini badala ya kununua zinazozalishwa nje siziso na ubora wa kutosha tena zenye gharama kubwa.
Search This Blog
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment