Search This Blog
Monday, March 30, 2020
Pasta Uganda Kortini kwa Kusema Corona Haipo Afrika
Mamlaka nchini Uganda zimemfungulia mashtaka na kumfunga muhibiri wa injili ambaye anatuhumiwa kukana uwepo wa virusi vipya vya corona barani Afrika, polisi wamesema leo.
Muhubiri huyo maarufu, Augustine Yiga, anatuhumiwa na waendesha mashtaka kuwa aliwaambia waumini wa kanisa la Ufufuo wa Kikristo Ijumaa na maneno yake kutangazwa na vituovya televisheni kuwa "nchini Uganda na barani Afrika hakuna virusi vya corona".
"Pasta Yiga wa Kanisa la Ufufuo wa Kikristo ameshtakiwa na yuko mahaburu kwa kufanya vitendo ambavyo vinaweza kusambaza Covid-19," Patrick Onyango, msemaji wa polisi, alisema.
"Kudai kwamba Covid-19 haipo Afrika wala Uganda kunafanya juhudi za serikali kupambana na ugonjwa huo wa dunia kuwa hazina maana na kunauweka umma katika hatari kubwa zaidi ya kutozingatia miongozi ya kudhibiti na kujikinga," alisema.
Lakini mwanasheria wa pasta huyo, Wilberforce Kayiwa, alisema Yiga alikana shtaka la kuendeleza maambukizi ya virusi hivyo.
Kiongozi huyo wa kidini anakabiliwa na kifungo cha hadi miaka saba jela, Yiga, ambaye anaendesha kanisa na kituo cha televisheni, ana wafuasi wengi na anajulikana kwa kutoa kauli zenye utata na kudai ana nguv u za kinabii.
Hadi sasa, Uganda imeripoti watu 33 wenye maambukizi ya virusi vya corona, Rais wa Uganda, Yoweri Museveni amewataka wananchi kubakia majumbani lakini hajatoa amri ya kutotoka nyumbani.
Shule, maeneo ya burudani na ya kuabudia na baadhi ya masoko ya bidhaa za kilimo, yamefungwa kwa muda wa mwezi mmoja na watu wamepigwa marufuku kusafiri kwa kutumia usafiri wa umma na kuwa zaidi ya watu watatu ndani ya gari, au zaidi ya mmoja katika pikipiki.
Wiki iliyopita, watu sita raia wa China na Waganda wawili walishtakiwa kwa kufanya kitendo ambacho kinaweza kusababisha kusambaa kwa maambukizi ya virusi hivyo baada ya kutoroka hotelini walikokuwa wamewekwa chini ya karantini.
Watu wawili kati ya raia hao wa China waligundulika kuwa na maambukizi.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment