Kiongozi mkuu wa kidini nchini Iran, Ayatollah Ali Khamenei amesema Iran haitopokea msaada wowote kutoka Marekani, katika kubadili hali ilivyo kutokana na wimbi la maambukizi ya virusi vya corona nchini mwake.
Katika taarifa yake hiyo Khamenei alirejea kuizungumzia dhana ya kwamba virusi hivyo ni silaha iliyoundwa na Marekani dhidi ya maadui zake.
Katika hotuba yake iliyorushwa moja kwa moja kupitia televisheni kiongozi huyo amesikika akisema wana maadui wengi lakini, mkubwa kuliko wote ni Marekani.. na sasa anataka kuwasaidia. Ni vyema taifa hilo likajikita katika kuwasaidia wananchi wake.
Iran limekuwa eneo tete la usambaaji wa virusi vya corona, ambavyo vilianzia China mwishoni mwa mwaka uliopita. Hata hivyo usambaaji wa visa hivyo ulianza kuingia Marekani wiki iliyopita.
Marekani inakabiliwa na mamia ya vifo vyenye kuhusishwa na virusi hivyo, wakati Iran vifo vyake vinapindukia watu 1000.
Katika hatua hiyo ya kukataa msaada, Khamenei aligusia nadharia ya kwamba virusi hivyo viliundwa na Marekani kwa lengo la kuyadhoofisha mataifa adui kama China na Iran.
Tangu Januari Khamenei amekiwa akisema virusi hivyo vinaweza kuwa silaha ya kibailojia iliyoundwa na Marekani.
Search This Blog
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment