Idadi ya vifo vilivyotokana na virusi vya Corona nchini Iran imeongezeka na kufikia 54 kulingana na wizara ya afya, huku pia visa vya maambukizi mapya navyo vikipanda usiku kucha hadi watu 978.
Taarifa ya wizara ya afya imesema maambukizi mapya yamethibitishwa kwenye miji kadhaa ikiwemo Mashhad, ambao ni mji ulio na maeneo matakatifu ya kishia yanayowaleta mahujai kutoka kanda nzima.
Idadi hiyo mpya inawakilisha vifo 11 zaidi ya vilivyoripotiwa Jumamosi na maambukizi makubwa ya watu 385.
Shirika la utangazaji la taifa la Iran limetangaza leo kwamba safari zote za ndege kuelekea jimbo la Gilan zimesitishwa.
Maeneo ya Gilan ndiyo yaliyo na maambukizi mengi baada ya Tehran na mji mtakatifu wa Qom.
Virusi hivyo vya Corona vilivyoanzia China vimeathiri maafisa saba wa serikali akiwemo makamu wa rais.
Search This Blog
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment